Friday, August 26, 2011

LIGI KUU YA VODACOM KUTIMUA TENA VUMBI HAPO KESHO

Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea tena kesho kwa mechi moja kati ya African Lyon na Toto Africans itakayochezwa Uwanja wa Chamazi ulioko Mbande, Dar es Salaam.
 
Agosti 28 mwaka huu kwenye uwanja huo huo kutakuwa na mechi kati ya JKT Ruvu na Kagera Sugar. Mechi nyingine kwenye Uwanja wa Chamazi itachezwa Agosti 30 mwaka huu kati ya Moro United na Toto Africans.
 
Mechi mbili zitachezwa Agosti 31 mwaka huu ambapo Mtibwa Sugar itakuwa mwenyeji wa Kagaera Sugar katika Uwanja wa Manungu, Morogoro wakati Villa Squad na Polisi Dodoma zitaumana kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment