Sunday, July 15, 2012

MATUKIO KATIKA PICHA YA UCHAGUZI WA KLABU YA YANGA UNAOENDELEA KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE MCHANA HUU!

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe akihutubian
 Chakula time
 Abel Mcharo aliyesoma dua ya Kikristo akisalimiana na Mussa Katabaro, pembeni yake kulia ni Clement Sanga, Yussuf Manji akisalimiana na Mzee aliyesoma dua ya Kiislamu na Abdallah Bin Kleb
  Godfrey Mabaga
 Mosha na Meja Ally Mayay Tembele kushoto
 Mzee Akilimali kulia
Serikali kuu; Manji na Sanga

 Saraha Ramadhan aliyeenguliwa, akiwa na John Jambele
Vijana wanaoendesha mchakato wa kura

UCHAGUZI Mdogo wa klabu ya Yanga, unafanyika leo kuanzia saa 5:00 asubuhi katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam huku kambi ya Yussuf Mehboob Manji ikipewa nafasi kubwa ya kushinda.
 
Manji anayewania Uenyekiti dhidi ya Edgar Chibura na John Jambele, juzi alitambulisha watu watano anaotaka kuchaguliwa nao leo wakati alipokuwa akihutubia mamia ya wanachama kwenye Mkutano wa kampeni, Uwanja wa Kaunda, uliopo makao makuu ya klabu, makutano ya Mitaa ya Twiga na Jangwani.
 
Manji aliwataja watu hao kuwa ni nafasi ya Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na Wajumbe wanne ni Abdallah Bin Kleb, Mussa Katabaro, Lameck Nyambaya na George Manyama.
Ikumbukwe uchaguzi huo mdogo unafuatia Wajumbe wengi wa Kamati ya Utendaji iliyochaguliwa miaka miwili iliyopita, akiwemo Mwenyekiti Wakili Lloyd Baharagu Nchunga na Makamu wake, Davis Mosha kujiuzulu na watakaochaguliwa Jumapili watadumu kwa miaka miwili, kumalizia kipindi cha uongozi cha waliojiuzulu.
 
Manji aliwaomba wanachama wa Yanga pamoja na kumchagua yeye Jumapili, pia wawachague na watu hao watano, Sanga, Katabaro, Bin Kleb, Nyambaya na Manyama, kwani ni watu ambao anaamini atafanya nao kazi vizuri na kwa ufanisi.
 
Alisema iwapo akichaguliwa watu hao na mambo yakawa mabaya klabuni, atakuwa tayari kujiuzulu lakini akasema atasikitika iwapo atachaguliwa pamoja na watu tofauti nao hao.
Alisema katika kipindi hiki ambacho klabu haina uongozi, watu hao watano wamekuwa wakimsaidia kujenga timu kama kusajili na kadhalika kwa kujitolea hivyo ana imani nao kwa kiasi kikubwa.
 
Shughuli hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa wanachama Vijana wa Yanga, Bakili Mohamed Makele na Mwenyekiti wa Wazee, Mzee Ibrahim Ally Akilimali, ambao waliwaomba wana Yanga kuchagua timu hiyo na mambo yatakuwa mazuri.
Umati wa wanachama wanaokadiriwa kufika 2000 au zaidi ulihudhuria mkutano huo na wakati wote walikuwa wakishangilia hotuba, kuonyesha kwamba wanaafiki.
PICHA KWA HISANI YA  http://bongostaz.blogspot.com/


TAARIFA KUTOKA TFF, LEO, JULAI 15, 2012!

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Julai 15, 2012
NGORONGORO, RWANDA KUUMANA JULAI 16

Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) itacheza mechi ya kirafiki na Rwanda itakayofanyika kesho (Julai 16 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo ya kujipima nguvu kwa Ngorongoro Heroes inayofundishwa na Kocha Jakob Michelsen kabla ya kucheza na Nigeria katika mechi za mchujo za michuano ya Afrika itaanza saa 10 kamili jioni.
Ngorongoro Heroes ambayo katika raundi ya kwanza ya michuano hiyo iliitoa Sudan itacheza mechi ya kwanza ya raundi ya pili Julai 29 mwaka huu dhidi ya Nigeria kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Rwanda ambayo inaundwa na wachezaji wengi waliocheza fainali za Kombe la Dunia kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 miaka mitatu iliyopita tayari iko nchini. Kikosi chake kina wachezaji 20 na viongozi saba.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 2,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani wakati VIP B na C itakuwa sh. 5,000. Kiingilio kwa VIP A itakuwa sh. 10,000.

MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI
Mjumbe wa Kamati ya Tiba ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Dk. James Sekajugo atakuwa na mkutano na waandishi wa habari leo mchana (Julai 15 mwaka huu).
Mkutano huo utafanyika saa 8 mchana kwenye ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Dk. Sekajugo kutoka Uganda yuko nchini kusimamia upimaji umri (MRI Test) kwa wachezaji wa timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) uliofanyika jana kwenye hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam.
Upimaji huo umefanyika kutokana na maagizo ya CAF kuwa wachezaji wote wanaoshiriki michuano ya Afrika kwa umri chini ya miaka 17 ni lazima wapimwe kipimo cha MRI Test ndipo waruhusiwe kucheza.
Serengeti Boys imepangiwa kucheza Septemba mwaka huu dhidi ya Kenya katika raundi ya kwanza ya michuano hiyo.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)