Wednesday, August 31, 2011

BARCELONA YAANZA NA MAUAJI LA LIGA, YAIKANDAMIZA VILLARREAL 5-0!

Wachezaji wa FC Barcelona wakishangilia kumpongeza Lionel Messi wa Argentina kufunga bao katika mechi yao ya ufunguzi ya Ligi Kuu Hispania, La Liga dhidi ya Villarreal kwenye Uwanja wa Camp Nou mjini Barcelona, Hispania jana Jumatatu. Barca ilishinda 5-0.
Barcelona waliifunga Villareal bila hururma kwa mabao 5-0 na kuwajibu wapinzani wao Madrid ambao waliwafunga Zaragoza mabao 6-0.
Pep Guardiola aliwakosa Dani Alves , Carles Puyol na Gerard Pique hivyo akamchezesha Eric Abidal na akawatumia Sergio Busquets na Javier Mascherano kwenye ulinzi.
Xavi Hernandez na David Villa waliwekwa benchi huku Thiago Alcantara, Cesc Fabregas na Alexis Sanchez wote wakianza .
Juan Carlos Garido alipanga timu ile ile ya Villareal iliyotegemewa na wengi ambapo Bruno Soriano alirudi kwenye sehemu yake ya kiungo baada ya kuwa amecheza kaka beki katikati ya wiki na Gonzalo Rodriguez alirudi kucheza beki.

Mchezo huu ulikuwa si wa ushindani kama ule uliozikutanisha timu hizi mwaka jana . Villareal walikuwa hawana mashambulizi kabisa na walifia mikononi mwa Barca kwa urahisi ambao hakuna aliyeutegemea. Wafungaji wa mabao hayo ni:
 
 
 
 

No comments:

Post a Comment