Friday, August 19, 2011

KUFUNGWA KWA UWANJA WA TAIFA KWAATHIRI LIGI KUU TANZANIA BARA INAYOANZA KESHO

Uamuzi huo wa uwanja kufungwa kwa ajili ya matengenezo pia umeziathiri klabu za Yanga na Simba ambazo zilikuwa zimekubaliwa timu zao ziutumie kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu ya Vodacom ambayo inaanza kutimua vumbi Agosti 20 mwaka huu.

Tayari leo (Agosti 18 mwaka huu) tumeziandikia rasmi klabu za Simba na Yanga tukizifahamisha kuhusu uamuzi huo wa Wizara, hivyo kuzitaka zitafute viwanja vingine kwa ajili ya mechi zao za ligi.

Hatua hiyo ya uwanja kufungwa, kutailazimisha TFF ifanye mabadiliko kwenye ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom kwa kuzingatia viwanja ambavyo klabu za Yanga na Simba zitakuwa zimeamua kuvitumia.

Mabadiliko hayo pia yataziathiri timu za African Lyon, Azam, JKT Ruvu, Moro United na Villa Squad ambazo licha ya kutumia Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam kwa mechi zao, zilipanga mechi zao za nyumbani dhidi ya Simba na Yanga zichezwe Uwanja wa Taifa.

Kwa sasa msimamo wa wamiliki wa Uwanja wa Azam ni klabu za Yanga na Simba kutoutumia kwa vile uwezo wake wa kuchukua watazamaji ni mdogo. 

No comments:

Post a Comment