Wednesday, August 31, 2011

HUKUMU YA RAGE NA SENDEU YAPIGWA KALENDA!

Ismail Aden Rage - Mwenyekiti wa Klabu ya Simba
Afisa habari wa klabu ya Yanga, Luis Sendeu (kushoto), Mwenyekiti wa Yanga Nchunga (katikati )na Makamu Mwenyekiti Mosha wakiwa klabuni Yanga
Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) chini ya Mwenyekiti wake Alfred Tibaigana iliyokuwa ikutane jana kusikiliza malalamiko dhidi ya Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage na Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu imeahirisha kikao chake.
 
Kwa mujibu wa Tibaigana, kikao kimeahirishwa kutokana na Kamati kutotimiza akidi (column) kwa wajumbe wake. Walalamikiwa wataarifiwa siku ambayo kikao kitapangwa tena.


No comments:

Post a Comment