Wednesday, August 31, 2011

JOE COLE ATUA LILE

JOE COLE
Kiungo wa Liverpool Joe Cole amejiunga na klabu ya Lille ya Ufaransa kwa mkopo kwa msimu huu.
Cole mwenye umri wa miaka alikwenda Ufaransa siku ya Jumanne kufanyiwa vipimo vya afya yake na licha ya kutakiwa pia na klabu ya Aston Villa, amechagua kujiunga na Ligi ya Ufaransa.
Mchezaji huyo anayechezea pia timu ya taifa ya England, alijiunga na Anfield mwezi wa Julai mwaka 2010 kwa mkataba wa miaka minne akitokea Chelsea lakini ameanza kucheza mechi 11 tu kwa Liverpool.
Hakuwa kucheza mechi hata moja tangu Kenny Dalglish achukue hatamu msimu huu.



No comments:

Post a Comment