Wednesday, January 4, 2012

MICHUANO YA KOMBE LA MAPINDUZI: SIMBA KAMA YANGA, YADUNGULIWA MISUMARI MIWILI KWA MMOJA NA JAMHURI YA PEMBA.


 Mashabiki wa soka wakifuatilia kwa umakini wa hali ya juu mchezo kati ya Simba na Jamhuri, katika michuano ya kombe la Mapinduzi, katika uwanja wa Amaan, Jamhuri walishinda magoli 2-1.
 Wachezaji wa Jamhuri wakishangiria goli lao la kwanza dhidi ya Simba, katika pambano lililopigwa katika uwanja wa Amaan usiku wa kuamkia leo, katika mfululizo wa michuano ya kombe la Mapinduzi yanayoendelea kisiwani Unguja (Picha zote na Ali Mohammed)
 Ubao wa matokeo ukisomeka SIMBA 0, JAMHURI 1, hapa ilikuwa ni dakika ya 11.

 Benchi la ufundi la timu ya Jamhuri wakifuatilia kinachoendelea kiwanjani.
Benchi la ufundi la Simba pamoja na wachezaji wa akiba wakiwa hawaamini kinachotokea uwanjani baada ya kushuhudia timu yao ikilazwa mabao 2-1 na Jamhuri, katika pambano lililosukumizwa katika uwanja wa Amaan usiku wa kuamkia leo.
Bingwa mtetezi wa Mapinduzi Cup Simba SC imefuata njia ya yanga katika michuano ya kombe la mapinduzi baada ya jana usiku kupokea kichapo cha goli 2-1 toka kwa Jamhuri ya visiwani Zanzibar.
Mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa Amani Zanzibar ulishuhudia timu zote zikienda mapumziko bila ya kutingisa nyavu, na kipindi cha pili ndipo mabao matatu yalishuhudiwa, huku mawili ya kitinga katika nyavu za wekundu wa Msimbazi Simba na moja likitinga katika nyavu za Jamhuri.
Katika mchezo wa awali ulishuhudi Miembeni ikitoka na ushindi wa goli moja bila dhidi ya KMKM, na hivyo kundi A likiwa linaongozwa na Jamhuri, ikifuatiwa na Miembeni na Simba ikiwa ya tatu.
Leo ni zamu ya yanga kuzinduka pale watakapo wakabili Kikwajuni na Azam FC kucheza dhidi ya Mafunzo katika michezo ya kundi B.