Monday, September 12, 2011

WAZIRI NUNDU ATOA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KWA RAIS WA ZANZIBAR

Waziri wa Uchukuzi  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Omar Rashidi Nundu.

Waziri wa Uchukuzi Mhe.Omar Rashidi Nundu,ametoa salamu za Rambi Rambi kutokana na vifo vya watu zaidi ya 200 vilivyotokea katika eneo la Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja iliyotokana na kuzama kwa Meli ya Mv Spice .
Akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari kwa niaba ya Katibu Mkuu Edward Mkiaru, Waziri Nundu alisema, Wizara imepokea taarifa hiyo kwa masikitiko na inawapa pole wafiwa wote pamoja na kuwaombea afya njema wale wote walionusurika katika ajali hiyo.
Aidha wizara imewashukuru wananchi wote walioshiriki kwa njia moja ama nyingine katika kuokoa wale waliofikwa na mkasa huo.
“Kutokana na tukio hili tunamuomba Mwenyezi Mungu awafariji wote waliofikwa katika kipindi hiki kigumu na pia azilaze roho za Marehemu wa ajali hiyo mahali pema peponi”alisema Mkiaru

No comments:

Post a Comment