Monday, September 12, 2011

DK. SHEIN AONGOZA MAMIA KATIKA DUA YA KUWAOMBEA WAATHIRIKA WA MELI YA MV SPICE ISLANDES

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(watatu kutoka kushoto) akijumuika na baadhi ya viongozi wa Serikali na wananchi wa Zanzibar katika dua ya pamoja ya kuwaombea marehemu waliofariki katika ajali ya meli iliyotokea mwishoni mwa wiki eneo la Nungwi,Unguja.Viongozi wengine katika picha kutoka kushoto ni Rais Mstaafu wa Zanzibar Amani Abeid Karume, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Seif Shariff Hamad,kushoto kwa Rais Kikwete ni Rais wa Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein,Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Mohammed Gharib Bilal,Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Rais Mstaafu awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi.
Baadhi ya wananchi wa Zanzibar wakiswali wkati wa dua maalumu ya kuwaombea marehemu waliofariki katika ajali ya meli ya Spice Islander iliyotokea mwishoni mwa wiki eneo la Nungwi,Unguja.Swala hiyo ya pamoja ilifanyika leo(sept 12) katika viwanja vya Maisara.

No comments:

Post a Comment