Wednesday, September 14, 2011

TIMU YA KIKAPU YAENDA NAIROBI

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), Mussa Mziya (kulia) akikabidhi bendera ya Taifa kwa nahodha wa timu ya wachezaji wa mpira wa kikapu chini ya miaka 16 Mrumbia Issa jijini Dar es Salaam Jana Jumanne Septemba 13, 2011. Timu hiyo imeondoka leo Jamatano Septemba 14, 2011 kwenda Nairobi, Kenya, kushiriki fainali za timu kutoka ukanda wa Coca-Cola wa Afrika Mashariki, Kati na Afrika Magharibi (CEWA). Nyota wa fainali hizo watachaguliwa kwenda Marekani kwenye mafunzo zaidi chini ya udhamini wa Coca-Cola kupitia kinywaji chake cha Sprite.

No comments:

Post a Comment