Sunday, September 4, 2011

SILAHA MPYA YA ARSENAL NI NOMA, YAPIGA HAT-TRICK!

Mchezaji mpya wa Arsenal Park Chu-Young.
Mchezaji mpya wa Arsenal Park Chu-Young, mchana wa leo ameiwezesha Nchi yake Korea Kusini kupata ushindi a magoli 6-0 dhidi ya Lebano.

Katika mchezo Park Chu-Young aliweza kufunga magoli matatu (hat-trick), huku magoli mengine yakifungwa na mshambuliaji mpya wa timu ya Sunderland Ji Dong-Won, huku mengine mawili yakifungwa na kiungo wa Timu ya Sangju Sangmu  Kim Jung-Woo.

Kwa ushindi huo Korea Kusini, imejiweka kwenye mwanzo mzuri wa kampeni yake, kuweza kupata tiketi ya kushiriki kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment