Wednesday, September 14, 2011

PAT RICE AWAPA MATUMAINI WAPENZI WA ARSNAL

Robin van Persie
Meneja msaidizi wa Arsenal Pat Rice, anaamini sare dhidi ya Borussia Dortmund katika mechi ya kwanza ya patashika za Ligi ya Ubingwa wa Ulaya ni muelekeo mzuri wa timu hiyo kuanza kubadilika msimu huu.
Arsenal walionekana wameshinda mechi hiyo na kuzoa pointi tatu katika Kundi F hadi dakika ya 88 ambapo Ivan Perisic aliisawazishia Dortmund.
Lakini Rice, alipoulizwa iwapo Arsenal sasa imeanza kubadilika alisema: "Sana tu.
"Inaonekana ni hivyo, hasa ushindi dhidi ya Swansea siku ya Jumamosi, ndio tulianza msimu. Wachezaji tulionao ni wazuri, wazuri sana, ni wachezaji wazuri sana." Aliongeza Rice.
Arsenal walikuwa na hali ngumu hasa robo ya msimu huu kufuatia kuyumbayumba katika mechi za ligi baada ya kutoka sare na Newcastle na baadae wakapoteza mechi dhidi ya Liverpool na Manchester United - ambapo katika uwanja wa Old Trafford walibugizwa mabao 8-2.
Hata kufuzu kwa Arsenal katika Ubingwa wa Ulaya walipoishinda Udinese kwa jumla ya mabao 3-1, bado timu ilikuwa ikiyumba.
Hata hivyo mwishoni mwa dirisha la usajili, wakati Cesc Fabregas na Samir Nasri walipouzwa na wakawasajili Per Mertesacker, Mikel Arteta na Yossi Benayoun, mechi ya Jumamosi ya Ligi Kuu ya England walipoishinda Swansea, Rice anaamini Arsenal sasa ipo katika mchakato wa kujengeka.
Na kocha huyo amekuwa na kauli ya matumaini kufuatia sare dhidi ya Dortmund.
Robin van Persie alionekana kuifagilia njia ya ushindi Arsenal katika mechi ya ufunguzi ya kundi la F kwa kumalizia vizuri pasi aliyotanguliziwa na Theo Walcott lakini bao maridadi la Perisic likawanyima Arsenal pointi tatu.
Naye kocha wa Dortmund Jurgen Klopp amesema timu yake ilistahili kupata sare baada ya jitahada kubwa walizofanya.
"Ilikuwa ni mechi nzuri, lakini wakati mwengine kandanda ndivyo ilivyo," alisema Klopp. "Tulicheza vizuri, vizuri sana kwa muda wote wa dakika 90.

No comments:

Post a Comment