Wednesday, September 28, 2011

AFRIKA KUSINI KUANDAA AFRICA CUP OF NATIONS 2013

MOJA YA VIWANJA VITAKAVYOTUMIKA KWENYE AFCON 2013
UWANJA WA CAPE TOWN 
Libya imeichia nafasi ya kuandaa mashindano hayo kutokana na hali kutokuwa shwari nchini humo.
Badala yake Libya itaandaa mashindano ya mwaka 2017, ambayo ilikuwa awali yafanyike nchini Afrika Kusini.
Kubadilishana huko ni makubaliano baina ya nchi hizo mbili ambayo yalifahamika wiki mbili zilizopita.
Wakati huo Caf ilisema tangazo hilo limetolewa mapema mno, huku Nigeria na Algeria pia zilionesha nia ya kuandaa.
Nigeria ilitajwa kuwa nchi itakayosubiri wakati Caf ilipotoa tangazo la awali kuhusu wapi mashindano ya kuuanzia mwaka 2010 - 2014 yatakapofanyika.
Lakini uamuzi wa kufanya mashindano hayo Afrika Kusini, uliidhinishwa na mkutano wa Kamati ya Utendaji ya Caf unaofanyika mjini Cairo.
Afrika Kusini pia itachukua nafasi ya Libya kuandaa michezo ya mwaka 2014 ya Mataifa ya Afrika, kwa wachezaji wanaotimua ligi za nyumbani.
Mapema mwaka huu waliandaa pia mashindano ya vijana ya Afrika chini ya miaka 20, ambayo Libya ilishindwa kuandaa.
Caf pia ilitangaza nchi mbalimbali zitakazoandaa mashindano kadha makubwa.
Namibia itandaa mashindano ya Wanawake ya mwaka 2014 ya Ubingwa wa Afrika na Niger itachukua jukumu la kuandaa mashindano ya mwaka 2015 chini ya umri wa miaka 17 .
Senegal itakuwa mwenyeji wa fainali za mwaka 2015 chini ya umri wa miaka 20, wakati Madagascar itakaribisha nchi nyingine katika kuwania ubingwa wa mashindano ya umri wa chini ya miaka 17 ya mwaka2017.

No comments:

Post a Comment