Wednesday, September 14, 2011

SIMBA, YANGA HEBU WAIGENI HAWA.....

Napenda niwaulize wadau kama kweli ni haki kwa Timu za Simba na Yanga kuufanya uwanja wa Azam FC kuwa kama uwanja wao wa nyumbani!! La hasha, kwa mimi nitasema si haki, ni kitendo cha aibu sana kwa timu hizi mbili kubwa ambazo kama tunavyojuaona ni jinsi gani zilivyo vilabu kongwe hapa nchini lakini havina viwanja vyao vya kuweza kucheza mechi zao za ligi za nyumbani na za kimataifa.
Tunawaomba Viongozi wa timu hizi mbili mlio madarakani kw sasa muone hili ni kama changamoto kwenu kwa timu changa imeweza kuwa na uwanja wake, na timu zenu zikajikuta mnaenda kucheza kwenye uwanja huo, ni fedheha sana kwenu.
"USHAURI WA BURE VIONGOZI JITAHIDINI KUJALI MASLAHI YA TIMU ZENU"

No comments:

Post a Comment