Tuesday, September 13, 2011

RIO FERDINAND AJIBU MASWALI YA MASHABIKI WAKE KWA NJIA YA TWITTER!

TWITTER Q&A NA RIO FERDINAND
Qn: Kama unapewa nafasi ya kuchagua kiungo bora kati ya Scholes, Gerrard, au Xavi utamchagua nani?
Rio: Paul Scholes a.k.a Satnav
Qn: Ni mafanikio makubwa unayojivunia katika maisha yako nje ya soka?
Rio: Namba 1 ni kupata uwezo wa kuwanunulia nyumba nzuri wazazi wangu.
Qn: Ni wachezaji gani ambao best professional na umewahi kucheza nao?
Rio: Gary Neville, Mikael Silvester na Ryan Giggs.
Qn: Uliumia zaidi kumuona mchezaji gani akihama Manchester United?
Rio: Cristiano Ronaldo, mchezaji bora, rafiki mzuri na alikuwa ananifurahisha sana, I miss him.
Qn: Mchezaji gani ambaye umewahi kupata tabu sana kumkaba katika soka?
Rio: Louis Saha ni kiboko alikuwa akinipa taabu sana zaidi tulipokuwa kwenye mazoezi ya Manchester United.
Qn: Top 3 ya viwanja ambavyo ni vigumu kucheza?
Rio: Uwanja wa Stoke, Middlesborough na Wolves, tena zaidi pitch zinapokuwa ngumu.
Qn: Mechi ngumu zaidi ya ugenini katika hatua ya makundi ya Champions league?
Rio: Mechi dhidi ya Villareal na ile dhidi ya Lille zilikuwa ngumu sana.
Qn: Kama ukipata nafasi ya kurudisha nyuma moja ya nyakati zilizopita katika maisha yako ndani ya soka, ungependa wakati upi ujirudie?
Rio: Mchezo wa fainali ya Champions league dhidi ya Chelsea in 2008, au mechi ya kwanza kuvaa na kucheza katika timu ya taifa na West Ham, au kufunga kwenye World Cup.
Qn: Je ungeendelea kucheza soka kama mishahara ya wachezaji wote itapunguzwa kuwa ya wastani mdogo?
Rio: Nitacheza kwa hali yoyote, haijalishi nalipwa kiasi gani.Naupenda huu mchezo.
Qn: Kiatu kipi unachokipenda zaidi na umewahi kukichezea?
Rio: Nike tiempo, kilaini na kipo comfortable kukichezea.
Qn: Nafasi gani unayopenda kucheza tofauti na ulinzi uwanjani?
Rio: No.10, kama Zidane au Bergkamp.

No comments:

Post a Comment