Wednesday, September 28, 2011

AFRIKA KUSINI KUANDAA AFRICA CUP OF NATIONS 2013

MOJA YA VIWANJA VITAKAVYOTUMIKA KWENYE AFCON 2013
UWANJA WA CAPE TOWN 
Libya imeichia nafasi ya kuandaa mashindano hayo kutokana na hali kutokuwa shwari nchini humo.
Badala yake Libya itaandaa mashindano ya mwaka 2017, ambayo ilikuwa awali yafanyike nchini Afrika Kusini.
Kubadilishana huko ni makubaliano baina ya nchi hizo mbili ambayo yalifahamika wiki mbili zilizopita.
Wakati huo Caf ilisema tangazo hilo limetolewa mapema mno, huku Nigeria na Algeria pia zilionesha nia ya kuandaa.
Nigeria ilitajwa kuwa nchi itakayosubiri wakati Caf ilipotoa tangazo la awali kuhusu wapi mashindano ya kuuanzia mwaka 2010 - 2014 yatakapofanyika.
Lakini uamuzi wa kufanya mashindano hayo Afrika Kusini, uliidhinishwa na mkutano wa Kamati ya Utendaji ya Caf unaofanyika mjini Cairo.
Afrika Kusini pia itachukua nafasi ya Libya kuandaa michezo ya mwaka 2014 ya Mataifa ya Afrika, kwa wachezaji wanaotimua ligi za nyumbani.
Mapema mwaka huu waliandaa pia mashindano ya vijana ya Afrika chini ya miaka 20, ambayo Libya ilishindwa kuandaa.
Caf pia ilitangaza nchi mbalimbali zitakazoandaa mashindano kadha makubwa.
Namibia itandaa mashindano ya Wanawake ya mwaka 2014 ya Ubingwa wa Afrika na Niger itachukua jukumu la kuandaa mashindano ya mwaka 2015 chini ya umri wa miaka 17 .
Senegal itakuwa mwenyeji wa fainali za mwaka 2015 chini ya umri wa miaka 20, wakati Madagascar itakaribisha nchi nyingine katika kuwania ubingwa wa mashindano ya umri wa chini ya miaka 17 ya mwaka2017.

Thursday, September 15, 2011

YANGA KATIKA MTIHANI MWENGINE KWA LYON LEO!



Yanga hii leo wanateremka kwenye nyasi bandia za Azam kumkabili African lyon katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara.
Yanga watakuwa wanasaka ushindi wao wa kwanza toka wamfunge simba katika fainali ya Kagame Cup, huku wakihangaika kujinasua toka mkiani. Leo watashuka bila ya mshambuliaji wake waliyo mfungia kwa utovu wa nidhamu Jerry Tegete.
Afican lyon watateremka katika dimba la Azam wakiwa na dhamira ya kuendelea kuitibulia yanga huku nao wakitaka kujiweka katika nafasi nzuri katika msimamo wa ligi kwa kuibuka na ushindi hii leo.
Katika mchezo uliochezwa jana Simba waliichapa goli moja timu ya Polisi Dodoma, goli lililo fungwa na Kago.


MSIMAMO WA VPL.Kwenye Mabano Idadi ya Mechi Zilizochezwa.
1. Simba SC (5) 13
2. JKT Ruvu (5) 9
3. Mtibwa Sugar ( 5) 8
4. Moro United (5) 8
5. Azam FC (5) 8
6. Toto Africa (5) 7
7. JKT Oljoro ( 5) 6
8. Africa lyon (4) 5
9. Coastal Union (5) 4
10. Villa Squad (5) 4
11. Kagera Sugar (5) 4
12. Ruvu Shooting (5) 4
13. Polisi Dodoma (5) 3
14. Yanga SC (4) 3

CHANGIA KUSAIDIA WAATHIRIKA WA AJALI YA MELI YA MV. SPICE ISLANDERS

Wednesday, September 14, 2011

BOAS: CHELSEA 'ITAITUNGUA' MAN UTD

Andre Villas Boas
Meneja wa Chelsea Andre Villas-Boas amekiri kikosi chake kitakabiliana na " changamoto tofauti" watakapojimwaga uwanja wa Old Trafford siku ya Jumapili kuikabili Manchester United.
David Luiz na Juan Mata walifunga mabao wakati Chelsea ilipoilaza Bayer Leverkusen mabao 2-0 wakati wa mechi yao ya ufunguzi kuwania Ubingwa wa Ulaya siku ya Jumanne.
Akiwa jicho moja ametumbulia mechi ya Jumapili, Villas-Boas alimpumzisha nahodha John Terry na Frank Lampard alikuwa katika benchi la wachezaji wa akiba.
Villas-Boas amesema: "Tutakwenda kujaribu kushinda. Itakuwa mechi nzuri sana nyakati hizi ligi ikiwa katika hatua za mwanzo."
Ameongeza: "Tunakabiliana na United pengine katika kipindi kizuri zaidi kilichojaa motisha, vipaji na mbinu nyingi za kupendeza za uchezaji.
Chelsea walionekana kun'gara muda mwingi wa mchezo dhidi ya timu hiyo ya Ujerumani, huku mshambuliaji anayechezea pia timu ya Taifa ya England chini ya umri wa miaka 21 Daniel Sturridge akiwa anaisumbua sana ngome ya Bayer Leverkusen kabla Luiz kufunga bao katika dakika ya 67 na Mata akaihakikishia ushindi kwa kupachika bao la pili zikiwa zimesalia dakika chache kabla mpira haujamalizika.
Matokeo hayo yamemfurahisha sana Villas-Boas, ambaye alisema: "Tulipata nafasi nyingi katika mchezo huo na tulistahili kushinda.

PAT RICE AWAPA MATUMAINI WAPENZI WA ARSNAL

Robin van Persie
Meneja msaidizi wa Arsenal Pat Rice, anaamini sare dhidi ya Borussia Dortmund katika mechi ya kwanza ya patashika za Ligi ya Ubingwa wa Ulaya ni muelekeo mzuri wa timu hiyo kuanza kubadilika msimu huu.
Arsenal walionekana wameshinda mechi hiyo na kuzoa pointi tatu katika Kundi F hadi dakika ya 88 ambapo Ivan Perisic aliisawazishia Dortmund.
Lakini Rice, alipoulizwa iwapo Arsenal sasa imeanza kubadilika alisema: "Sana tu.
"Inaonekana ni hivyo, hasa ushindi dhidi ya Swansea siku ya Jumamosi, ndio tulianza msimu. Wachezaji tulionao ni wazuri, wazuri sana, ni wachezaji wazuri sana." Aliongeza Rice.
Arsenal walikuwa na hali ngumu hasa robo ya msimu huu kufuatia kuyumbayumba katika mechi za ligi baada ya kutoka sare na Newcastle na baadae wakapoteza mechi dhidi ya Liverpool na Manchester United - ambapo katika uwanja wa Old Trafford walibugizwa mabao 8-2.
Hata kufuzu kwa Arsenal katika Ubingwa wa Ulaya walipoishinda Udinese kwa jumla ya mabao 3-1, bado timu ilikuwa ikiyumba.
Hata hivyo mwishoni mwa dirisha la usajili, wakati Cesc Fabregas na Samir Nasri walipouzwa na wakawasajili Per Mertesacker, Mikel Arteta na Yossi Benayoun, mechi ya Jumamosi ya Ligi Kuu ya England walipoishinda Swansea, Rice anaamini Arsenal sasa ipo katika mchakato wa kujengeka.
Na kocha huyo amekuwa na kauli ya matumaini kufuatia sare dhidi ya Dortmund.
Robin van Persie alionekana kuifagilia njia ya ushindi Arsenal katika mechi ya ufunguzi ya kundi la F kwa kumalizia vizuri pasi aliyotanguliziwa na Theo Walcott lakini bao maridadi la Perisic likawanyima Arsenal pointi tatu.
Naye kocha wa Dortmund Jurgen Klopp amesema timu yake ilistahili kupata sare baada ya jitahada kubwa walizofanya.
"Ilikuwa ni mechi nzuri, lakini wakati mwengine kandanda ndivyo ilivyo," alisema Klopp. "Tulicheza vizuri, vizuri sana kwa muda wote wa dakika 90.

KAGO AIPAISHA TENA SIMBA

Uhuru Suleimani wa Simba (kushoto) akiruka daluga la beki wa Polisi Tanzania, Nassor Mhagama.
Shujaa wa Msimbazi, Gervas Kago.
Katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliochezwa kwenye uwanja wa Azam,uliopo Chamazi jijini Dar-es-Salaam. Simba imeshinda 1-0.

REAL MADRID KUINGIA NA 'UZI' MWEKUNDU LIGI YA MABINGWA ULAYA

MASHABIKI WA LIVERPOOL WATAFURAHI KUMONA KIPENZI CHAO XABI ALONSO NDANI YA JEZI NYEKUNDU TENA